Timu ya mpira wa kikapu ya Polisi nchini Tanzania imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Kikapu baada ya kuifunga Nyuki vikapu 65 – 47 katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Mao Zedong visiwani Zanzibar. Mpaka wakati wa mapumziko, Polisi walikuwa wakiongoza kwa vikapu 32 – 17, na mpaka mchezo unamalizika, Polisi waliibuka videdea kwa kuwa na vikapu 65 – 47.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |