Kenya imezindua kipindi cha tatu cha mapambano dhidi ya nzige wa jangwani ambao wameenea katika kaunti 26 nchini humo na kuleta tishio jipya kwa usalama wa chakula na maisha ya vijijini.
Waziri wa Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Umwagiliaji Bw. Peter Munya amesema serikali imetenga fedha za ziada kwa ajili ya kununua vifaa na dawa za kuulia wadudu hao.
Pia amesema serikali ya nchi hiyo inashirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa FAO kujenga kituo cha operesheni katika sehemu ya kaskazini, na kuongeza mwitikio kwa uvamizi wa nzige.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |