Takwimu mpya zinaonesha kuwa idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa COVID-19 barani Afrika imefikia 116 katika nchi 12. Kati ya nchi hizo, watu 20 wamegunduliwa nchini Algeria, wawili wawili nchini Burkina-Faso, Cameroon, mmoja Togo, 59 nchini Misri (kifo kimoja), watano nchini Morocco (kifo kimoja), wawili nchini Nigeria, wanne nchini Senegal, 13 nchini Afrika Kusini, sita nchini Tunisia, mmoja nchini DRC na mmoja nchini Côte d'Ivoire.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |