• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya imetenga Sh500m kuokoa sekta ya Utalii

    (GMT+08:00) 2020-03-12 18:44:00

    Kenya imetenga Kenya Sh500 milioni kuisaidia sekta ya utalii kupambana na athari za mlipuko wa virusi vya Corona ambao sasa unahatarisha uchumi wa dunia.

    Waziri wa Utalii na Wanyamapori Najib Balala alisema sehemu ya fedha hizo zitatumika kurudisha imani na kuhakikisha kuwa Kenya inabaki kuwa eneo linalopendwa kwa usafiri duniani.

    Fedha nyingine zitatumika katika mkakati wa ufufuaji wa masoko makuu ya watalii wanaokuja Kenya.

    Waziri Balala aliyasema hayo jana wakati akihutubia wadau wa sekta ya utalii jijini Nairobi.

    Mkutano huo uliandaliwa na Wizara ya Utalii kujadili utayari wa serikali ya Kenya kuhusiana na sekta hiyo kufuatia janga la kimataifa la COVID-19.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako