Wachezaji watano wa Valencia na wafanyakazi wamegunduliwa kuwa na virusi vya korona. Hata hivyo wote wapo kwenye hali nzuri. Mlinzi wa Valencia na Argentina Ezequiel Garay amekuwa mchezaji wa kwanza wa La Liga kutangaza kuwa ana virusi hivyo mapema Jumapili. La Liga ya Hispania ilisimamishwa Alhamisi baada ya kikosi cha Real Madrid kuwekwa karantini. Hispania ni nchi ya pili kwa kuwa na maambukizi mengi ya korona katika Ulaya baada ya Italia, na inapanga kutangaza kufunga nchi nzima Leo Jumatatu
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |