Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) limesema, karibu watoto milioni 4.8 wamezaliwa nchini Syria tangu mapambano yalipoanza miaka 9 iliyopita. Watoto milioni moja wamezaliwa kama wakimbizi katika nchi jirani, na wanaendelea kukabiliwa na matokeo mabaya yanayoletwa na vita ya kikatili. Kwa mujibu na takwimu za kuanzia mwaka 2014 ufuatiliaji rasmi ulipoanza hadi mwaka 2019, watoto 5,427 walithibitishwa kuuawa, na wengine 3,639 kujeruhiwa katika mapambano; karibu watoto 5,000 walitumikishwa kwenye mapambano; na karibu mashirika 1,000 ya elimu na matibabu yameshambuliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |