Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amesema nchi yake imejenga ushirikiano wa kiwenzi na kampuni ya Alibaba ya China ili kuimarisha mapambano dhidi ya COVID-19.
Kwenye taarifa iliyotolewa Bw. Ahmed amesema makubaliano ya ushirikiano yamefikiwa baada ya mazungumzo kati yake na mkurugenzi wa kampuni ya Alibaba Bw. Jack Ma jana asubuhi. Amesema Ethiopia inamshukuru Bw. Jack Ma kwa kutoa vifaa 20,000 vya upimaji wa COVID-19 na mask zaidi ya 100,000 kwa Ethiopia, na kuishukuru Alibaba kwa kusambaza vitabu vya mwongozo wa kinga na tiba dhidi ya COVID-19.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |