Watu 15 wamefariki baada ya bomba la mafuta na gesi kulipuka jana asubuhi mjini Lagos, Nigeria.
Habari kutoka idara ya usimamizi wa mambo ya dharura ya Nigeria zimesema, mlipuko huo uliotokea saa tatu asubuhi kwa saa za huko, pia ulisababisha kuharibika kwa majengo zaidi 50.
Hivi sasa moto huo ulidhibitiwa na kazi za uokoaji inaendelea, na uchunguzi unaendelea ili kujua chanzo cha mlipuko huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |