Bunge la awamu ya 23 la Israel limeapishwa katika hafla ambayo wabunge waliapishwa kwa vikundi vya watu watatu watatu, ili kuendana na matakwa ya Israel kuhusu ukubwa wa mikutano wakati wa kukabiliana na maambukizi ya virusi vya korona. Rais Reuven Rivlin wa Israel amesema kwenye hafla hiyo kuwa, hivi sasa msukosuko wa kisiasa nchini Israel ni "wa kweli", na ametoa wito kwa vyama mbalimbali vya bunge kufikia maafikiano ili kuunda serikali mpya haraka iwezekanavyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |