Mkurugenzi wa IMF Bibi Kristalina Georgieva amesema IMF iko tayari kutoa mkopo wa dola za kimarekani trilioni 1 ili kuzisaidia nchi wanachama kupambana na msukosuko uliosababishwa na COVID-19.
Bibi Georgieva amesema ikiwa ni mstari wa kwanza wa kinga, IMF inaweza kutumia njia zake za dharura za kulipa kwa unyumbufu na haraka, kuzisaidia nchi zenye mahitaji ya dharura ya kutoa na kupokea fedha ya kimataifa. Njia hizo zinaweza kutoa fedha karibu dola za kimarekani bilioni 50 kwa nchi zinazoibuka kichumi. Nchi wanachama zenye mapato ya chini zinaweza kupata mkopo wa dola za kimarekani bilioni 10 bila riba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |