Mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Ulaya Bibi. Ursula von der Leyen amesema ili kupungua maambukizi ya COVID-19, Umoja huo umependekeza kuwekwa vizuizi vya usafiri usio lazima kwa watu kutoka nje ya umoja huo.
Baada ya kuhudhuria mkutano wa video wa viongozi wa kundi la nchi 7, Bibi von der Leyen amesema wanapendekeza kuzuia kwa muda usafiri usio lazima kwa watu kutoka nje ya Umoja wa Ulaya. Lakini raia wa nchi za Umoja wa Ulaya, wafanyakazi wa matibabu na wanasayansi wanaoshughulikia maambukizi ya virusi hiyo hawatazuiwa. Vizuizi hivyo vitakuwa vya muda, na kipindi cha awali ni siku 30. Viongozi wa nchi za Umoja wa watafanya mkutano kwa video leo kujadili pendekezo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |