Luc Eymael ambaye ndiye mwenye kauli ya mwisho kwenye benchi la ufundi la Yanga, amefunguka kuwa wapinzani wao Simba ni timu bora. Kocha huyo raia wa Ubelgiji, ameweka bayana kwamba Simba ni timu bora kwa sababu licha ya kwamba waliwafunga kwa bao 1-0 lakini mechi yao iliyofuata waliibuka tena na wakashinda kwa mabao 8-0 tofauti na wao ambao walipoteza kwa bao 1-0 dhidi ya KMC. Eymael amesema kuwa ubora wa Simba ulionekana baada ya kuwafunga lakini wakasimama na kufanya vizuri kwenye mechi yao iliyokuja katika ligi kuu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |