Rais Donald Trump wa Marekani amesema nchi hiyo inaweza kukabiliwa na mlipuko wa virusi vipya vya korona (COVID-19) mpaka mwezi Julai au Agosti, na kwamba uchumi wake huenda ukaporomoka.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ikulu hapo jana, rais Trump amesema makadirio ya ukuaji wa uchumi nchini humo yanaweza kurudi kwa nguvu. Pia ametoa mwongozo unaokataza mkusanyiko wa watu zaidi ya 10.
Wakati huohuo, Vituo vya Kudhibiti na Kukinga Magonjwa (CDC) nchini Marekani vimetoa ushauri kwa umma kufuta ama kuahirisha mikutano ya watu zaidi ya 50 katika wiki nane zijazo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |