Wizara ya afya ya Ethiopia imesema, mwanadiplomasia wa Uingereza amekuwa mgonjwa wa sita aliyethibitishwa kuambukizwa COVID-19 nchini Ethiopia.
Wizara hiyo imetoa taarifa ikisema, mwanadiplomasia mwanaume mwenye umri wa miaka 59 kutoka Uingereza, amekuwa mgonjwa wa sita wa COVID-19 nchini humo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwanadiplomasia huyo aliyerudi hivi karibuni kutoka Dubai amewekwa kwenye karantini jumatatu wiki hii baada ya kuonesha dalili za COVID-19. Alithibitishwa kuambukizwa baada ya kufanyiwa upimaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |