Iran jana iliripoti watu 1,178 zaidi waliothibitishwa kuambukizwa COVID-19 na vifo vya watu 135 kutokana na virusi hivyo, na kuifanya idadi ya jumla ya vifo kutokana na COVID-19 nchini humo ikaribie 1,000.
Wizara ya afya na elimu ya matibabu ya Iran imetangaza kuwa maambukizi ya COVID-19 yameongezeka na kufikia 16,169, na idadi ya vifo imefikia 988.
Qatar jana imeripoti watu watatu waliothibitishwa kuambukizwa COVID-19, na idadi ya jumla ya maambukizi nchini humo imefikia 442.
Uturuki imeripoti kifo cha kwanza na maambukizi 51 zaidi ya COVID-19, na idadi ya maambukizi nchini humo imefikia 98. Israel pia imesema idadi ya maambukizi ya COVID-19 nchini humo imefikia 337.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |