Waziri mkuu mteule wa Iraq Bw. Adnan al-Zurfi ameahidi kufanyika kwa uchaguzi huru na wa haki na wazi, kwa kushirikiana na Tume ya Umoja wa Mataifa nchini humo, ndani ya mwaka huu baada ya kuundwa kwa serikali mpya. Pia ameahidi kupambana na ufisadi katika wizara na taasisi nyingine za Iraq, na kuwasilisha bajeti ya mwaka 2020 kwenye bunge haraka iwezekanavyo baada ya kukagua njia za kuongeza mapato na kupunguza matumizi yasiyofaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |