Uongozi wa Yanga umeanza kuchukua hatua za tahadhari ya kujikinga na virusi vya korona kwa wachezaji pamoja na mashabiki. Afisa habari wa klabu hiyo, Hassan Bumbuli amesema wameanza kuchukua tahadhari katika mazoezi yao yanayofanyika katika Chuo cha Sheria jijini Dar es Salaam kwa kudanya mazoezi bila ya kuwepo kwa mashabiki. Licha ya hatua hiyo, bado timu hiyo inaendelea kuchukua tahadhari na ushauri unaotolewa na madaktari juu ya virusi hivyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |