Katika barabara hiyo, wafanyabiashara hao wanapaswa kupanga bidhaa zao kuanzia saa 10:00 jioni baada ya muda wa kazi kuisha, lakini wameonekana kukiuka utaratibu huo na kuanza kupanga kabla ya muda huo.
Onyo hilo lilitolewa jana na Ofisa Masoko wa Jiji la Dodoma, James Yuna, alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara hao wanaofanya biashara katika eneo hilo.
Alisema hivi sasa wamekuwa wakipanga bidhaa muda wa asubuhi hali inayoleta usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |