Mkurugenzi mkuu wa Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF Henrietta Fore amesisitiza umuhimu wa kuwalinda watoto wakati wa kukabiliana na COVID-19. Bibi Fore ametoa taarifa ikisema, kazi ya kuokoa maisha inayolenga kutoa afya, elimu, lishe na ulinzi kwa watoto imekuwa muhimu zaidi. Kufuatia mamilioni ya watoto kupoteza makazi na kuathiriwa na vita, kufariki kutokana na vyanzo vinavyozuilika, kukosa shule au kukosa chanjo za lazima, mahitaji ya uungaji mkono yamekuwa makubwa zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |