Huenda Liverpool haitapewa ubingwa wa Ligi Kuu England ikiwa tatizo la virusi vya korona litalazimisha msimu kumalizika kabla ya mechi zote kutimia kama ilivyothibitishwa na Rais wa Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA) Aleksander Caferin. Virusi hivyo vimesababisha kusimamishwa kwa muda kwa Ligi hiyo hadi April 5, huku Liverpool ikiwa inaongoza kwa tofauti ya point 25, lakini wataalam wanaamini kuwa hali itakuwa mbaya zaidi katika siku za usoni, jambo linaloleta wasiwasi kama msimu huu unaweza kumalizika au la.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |