• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jeshi la serikali ya Libya laimarisha udhibiti wake kusini mwa Tripoli dhidi ya waasi

    (GMT+08:00) 2020-03-19 17:51:55

    Msemaji wa jeshi la serikali ya Libya inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa Bw. Mohamed Gonono amesema jeshi hilo lilizuia shambulizi lililofanywa kusini mwa Tripoli na waasi wanaotokea sehemu ya mashariki ya nchi hiyo.

    Katika taarifa yake, Bw. Gonono amesema jeshi hilo liliwazuia wapiganaji wa kundi la waasi linaloongozwa na kamanda Jenerali Khalifa Haftar katika mji wa mashariki wa nchi hiyo, waliovunja azimio la kusitisha vita na kufanya mashambulizi kwa kutumia makombora huko Ain Zara, kusini mwa Tripoli.

    Kamanda wa jeshi la serikali Ahmad Abu-Shahma aliwaambia waandishi wa habari kuwa jeshi hilo limedhibiti tena eneo la Ain Zara.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako