Baraza la maua la Kenya limesema maambukizi ya COVID-19 yanayoendelea yamepunguza kwa asilimia 80 mauzo ya maua ya Kenya na sekta hiyo inatarajia kurejeshwa kwa safari za ndege za mizigo kwenda China katika wiki tatu ijayo. Mkurugenzi mkuu mtendaji wa baraza hilo Bw. Clement Tulezi, amesema hivi sasa Kenya inaweza kuuza tu maua kwa Uingereza na Ujerumani barani Ulaya, ambayo inachukua zaidi ya asilimia 70 ya mapato yote ya mazuo ya maua kwa nchi za nje.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |