Umoja wa Afrika umemwapisha Bw. Wamkele Mene kuwa katibu mkuu wa sektretarieti ya Makubaliano ya Eneo la Biashara Huria la Bara la Afrika huko Accra, mji mkuu wa Ghana, ambayo itakuwa makao makuu ya makubaliano hayo. Ikiwa moja kati ya majukumu yake, katibu mkuu huyo anatarajiwa kuhakikisha hatua za utekelezaji wa makubaliano, zinazotakiwa kuwa tayari kabla ya Julai mosi mwaka huu, ambayo utekelezaji wake utaanza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |