Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Geng Shuang amesema, China haitasahau misaada iliyotolewa na jamii ya kimataifa wakati ilipokumbwa zaidi na mlipuko wa virusi vya Corona (COVID-19).
Amesema hadi sasa serikali ya China imetangaza kutoa misaada kwa nchi na mashirika 82 ya kimataifa ikiwemo Shirika la Afya Duniani na Umoja wa Afrika.
Geng amesema misaada hiyo ni pamoja na maboksi ya kupima virusi vya Corona, mask, na mavazi ya kukinga virusi, pia China imefanya mikutano kwa njia ya video na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, ili kueleza uzoefu wake wa kupambana na COVID-19.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |