Aliyekuwa kiungo wa kati wa Man United, Marouane Fellaini amejiunga na orodha ya wanasoka ambao wamepata maambukizi ya virusi vya corona. Fellaini aliondoka United mwaka jana na kuhamia ligi ya China ya Super League. Mchezaji huyo anadaiwa kuwasili Jinan kwa mazoezi Ijumaa iliyopiota kwa usafiri wa treni wakati alipogundiliwa kuwa na virusi hivyo. Ligi hiyo ya China kama nyingine kote ulimwenguni kwa sasa imesimamishwa huku taifa hilo likikabiliana na janga hilo la kimataifa ambalo limeangamiza maelfu ya watu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |