Mkongwe ndani ya Liverpool, John Barnes amemshauri nyota wa Tottenham Hotspur, Harry Kane kubaki ndani ya timu hiyo. Kumekuwa na taarifa kwamba nyota huyo anampango wa kuibukia ndani ya Manchester United ili kupata changamoto mpya na kusaka makombe. Barne amesema Kane hatakiwi kuondoka Spurs kwa sababu kama anatafuta makombe wachezaji wengi wangehama klabu zao anachotakiwa kwa sasa ni kutulia na kufanya kazi ndani ya klabu yake ya Spurs. Spurs kwenye msimamo ipo nafasi ya nane ikiwa imecheza mechi 29 na ina pointi 41.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |