Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS imetangaza marufuku ya siku saba kwa wafanyakazi wa kigeni kwenda Sudan Kusini, ili kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona. Tume hiyo imetoa taarifa ikisema, njia hiyo itasaidia kuzuia kuenea kwa virusi nchini Sudan Kusini, ikiwa sehemu ya uungaji mkono unaotolewa na tume hiyo kwa juhudi za Sudan Kusini za kuzuia maambukizi ya COVID-19.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |