Benki za Afrika Kusini zimetoa likizo ya miezi mitatu ya kuahirisha ulipaji mikopo kwa makampuni madogomadogo na yenye ukubwa wa kati na wanafunzi kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona. Benki ya FNB imetoa taarifa ikisema, imesisitiza tena ahadi yake kwa makampuni madogomadogo na yenye ukubwa wa kati ambayo hali zao za kifedha zinaathiriwa na mlipuko wa virusi vya Corona. Benki hiyo inaendelea kushirikiana na chama cha benki cha Afrika Kusini, Benki Kuu ya Afrika Kusini na serikali ya nchi hiyo kutafuta utatuzi kwa njia mbalimbali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |