Timu ya wasichana ya Isiolo Starlets itakuwa miongoni mwa vikosi saba vitakavyoshiriki fainali za kitaifa kuwania taji la Chapa Dimba na Safaricom Season Three nchini Kenya mwaka huu. Kwa mara ya kwanza vigoli hao watakuwa wakiwakilisha Mkoa wa Mashariki baada ya kushinda kwenye fainali zilizopigiwa uwanjani Kenyatta Stadium, Machakos. Kocha wa timu hiyo Hussein Wako alisema kuwa mlipuko wa virusi hatari vya korona umewanyima nafasi ya kuendelea na mazoezi yao lakini hawana budi ila watasubiri wakati wa Mungu hali itakaporejea kawaida.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |