Mkurugenzi wa Benki ya Dunia Bw. David Malpass amesema, benki hiyo imemaliza mpango wa kutoa dola bilioni 160 za kimarekani katika uungaji mkono wa kifedha kwa nchi zilizoathiriwa vibaya na virusi vya Corona. Kwenye mkutano usio rasmi wa kundi la nchi 20 uliofanyika kwa njia ya video, Bw. Malpass amesema mpango huo unalenga kupunguza muda wa kurejesha hali ya kawaida, kujenga mazingira kwa ukuaji, kuunga mkono makampuni madogomadogo na yenye ukubwa wa kati, na kusaidia kuwalinda watu maskini na wenye hali duni ya kiuchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |