Kwa mujibu wa Kituo cha Sayansi na Uhandisi CSSE kwenye Chuo Kikuu cha Johns Hopkins, watu 82,404 wameripotiwa kuambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani, na kuifanya Marekani kuwa nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu walioambukizwa virusi hivyo duniani. Idadi ya watu walioambukizwa virusi hivyo imeongezeka kwa zaidi ya watu elfu kumi ndani ya saa tano nchini Marekani.
Takwimu kutoka CSSE zimeonesha kuwa, idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona imefikia 526,044 duniani, na 23,709 wamefariki kwa virusi hivyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |