Kiungo mkabaji wa Yanga, Papy Tshishimbi raia wa DRC, ametoa kauli ya matumaini Jangwani kwa kutamka kuwa bado mchezaji halali wa timu hiyo huku akiwaambia hakuna chochote kinachoendelea kati yake na watani wao Simba. Kauli hiyo aliitoa jana baada ya tetesi nyingi kuzagaa mitandaoni kuwa yupo kwenye hatua za mwisho za mazungumzo na Simba kwa ajili ya kusaini mkataba wa kuichezea timu hiyo. Hiyo imekuja baada ya kushindwa kufikia muafaka mzuri na viongozi wa Yanga katika kuongeza mkataba wa mwaka mmoja wa kuendelea kwenye timu hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |