• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mitumba yapigwa marufuku

    (GMT+08:00) 2020-03-27 20:01:32
    SERIKALI imepiga marufuku uagizaji wa nguo zilizotumika, almaarufu mitumba, kama sehemu ya mikakati ya kuzuia kuenea kwa virusi vya corona.

    Kwenye taarifa kwa vyombo vya habari Waziri wa Biashara na Ustawi wa Kiviwanda Betty Maina alisema kando na kuokoa maisha ya Wakenya hatua hiyo inalenga kulinda viwanda vya kutengeneza nguo vya humu nchini. Marufuku hii ambayo inaathiri wafanyabiashara wengi wa mitumba nchini Kenya, imejiri wakati ambapo waziri wa Afya Mutahi Kagwe kutangaza kuwa idadi ya watu walioambukizwa nchini humo imepanda hadi 31.

    Hii ni baada ya watu wengine watatu kugunduliwa kuwa na virusi hivyo kufikia Alhamisi.

    Bw Kagwe amesema visa vya maambukizi vimeathiri zaidi kaunti za Nairobi, Mombasa, Kilifi na Kwale.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako