Waziri wa mambo ya nje wa Iran Bw. Mohammad Javad Zarif ameilaani Marekani kuendelea na vikwazo dhidi ya Iran wakati wa mlipuko wa virusi vya Corona. Ameeleza kuwa vita vya kiuchumi vinavyofanywa na Marekani dhidi ya Iran vimebadilika kuwa "ugaidi wa kimatibabu" wakati wa mlipuko wa virusi vya Corona, hata limezidi kiwango kinachoruhusiwa kwenye medani ya vita. Bw. Zarif ameihimiza jumuiya ya kimataifa kupuuza vikwazo haramu vya Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |