Serikali ya mji wa Wuhan imesema hospitali 61 zilizoteuliwa kuwatibu wagonjwa wa COVID-19 zimefunguliwa tena kwa umma baada ya kusafishwa kwa dawa.
Naibu katibu mkuu wa serikali Bw. Li Tao amesema hospitali nyingine tano pia zitaanza kuwapokea wagonjwa wasio wa COVID-19 katika siku zijazo.
Bw. Li amesema kuwa kutokana na idadi ya wagonjwa wa COVID-19 katika mji huo kuendelea kupungua, wagonjwa wa COVID-19 wamehamishwa katika hospitali za kiwango cha juu ili kupata matibabu kwa pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |