Uongozi wa Simba chini ya Mohammed Dewji umeweka ofay a Shilingi milioni 85 na gari kwa beki wa kati wa timu ya Coastal Union, Bakari Nondo Mwamnyeto ili ajiunge na timu hiyo. beki huyo wa kati wa Coatal ambaye pia ni nahodha wa timu hiyo, msimu huu amekuwa kwenye kiwango kizuri kiasi cha kupata nafasi ya kuanza kwenye kikosu cha timu ya Taifa Tanzania Taifa Stars chini ya kocha Etienne Ndayiragije. Usajili wa beki huyo unatokana na ombi la kocha mkuu wa Simba Sven Vandelbroek kwa kuwa safu yake ya mabeki ina wachezaji wakongwe ambao wanaruhusu magoli mengi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |