Takwimu kutoka kituo cha kinga na udhibiti wa magonjwa cha Afrika zinaonyesha kuwa, hadi kufikia jana, idadi ya vifo kutokana na virusi vya Corona barani humo imefikia 172, huku idadi ya watu walioambukizwa virusi hivyo ikifikia 5,255.
Takwimu pia zinaonyesha kuwa nchi 47 kati ya nchi wanachama 55 wa Umoja wa Afrika zimeripoti maambukizi, na zilizoathiriwa vibaya zaidi ni Afrika Kusini yenye maambukizi 1,326, Misri 656 na Algeria 582. Aidha watu karibu 371 walioambukizwa virusi hivyo wamepona.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |