Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Hua Chunying amesema, hatua zilizochukuliwa na China zimebadilisha mchakato hatari wa maambukizi ya virusi vya Corona, na China itaendelea kufanya ushirikiano wa kimataifa dhidi ya virusi hivyo, ili kulinda usalama wa afya wa kikanda na kimataifa.
Jarida la Sayansi limechapisha ripoti iliyotolewa na wanasayansi wa Marekani, Uingereza na China, ikisema kama China isingechukua hatua hizo, kesi za maambukizi ya virusi vya Corona nje ya Wuhan nchini China zingepita laki saba. Ripoti hiyo inaona kuwa, hatua madhubuti zilizochukuliwa na China zilifanikiwa kuvunja mnyororo wa maambukizi ya virusi, na kutoa fursa nzuri kwa sehemu nyingine kujiandaa kukabiliana na COVID-19.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |