Rais Donald Trump wa Marekani amesema anakaribisha juhudi za China kutoa vifaa vya kinga kwa nchi na sehemu zilizokumbwa na COVID-19.
Alipoulizwa kama China "inachukua nafasi ya uongozi duniani" katika mapambano dhidi ya COVID-19, rais Trump amesema China kuzisaidia nchi zingine kutasaidia mapambano dhidi ya ugonjwa huo.
Rais Trump amesema hivi sasa nchi 151 zimekumbwa na COVID-19, na ameeleza matumaini yake kuwa China na nchi nyingine zenye vifaa vya ziada vya matibabu zitavitoa kwa nchi zenye mahitaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |