Tovuti ya serikali ya Uingereza imetoa taarifa ikisema kutokana na athari zinazoletwa na maambukizi ya virusi vya Corona, mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa uliopangwa kufanyika mwezi wa Novemba huko Glasgow utaahirishwa hadi mwakani. Taarifa hiyo pia imesema, kutokana na maambukizi hayo, kamati ya uenyekiti na pande husika zimefanya mazungumzo na kutoa uamuzi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |