Uingereza imesema itaahirisha mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa (COP26) uliopangwa kufanyika Novemba mwaka huu hadi mwakani kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona.
Taarifa iliyotolewa na serikali ya nchi hiyo imesema, tarehe mpya ya kufanyika mkutano huo mwaka ujao huko Glasgow chini ya mwenyeji Uingereza kwa kushirikiana na Italia zitatajwa baadaye baada ya majadiliano ya pande husika.
Taarifa hiyo imesema, uamuzi huo umechukuliwa na wawakilishi wa Tume ya Mfumo wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa pamoja na wajumbe kutoka Uingereza na Italia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |