• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakenya zaidi ya 500,000 hawakuwa na kazi mwaka jana-KNBS

    (GMT+08:00) 2020-04-02 20:40:38
    Wakenya takriban 500,000 wamezurura kwa zaidi ya mwaka mmoja wakitafuta kazi bila mafanikio.

    Haya ni kwa mujibu wa Ripoti mpya ya kazi iliyotolewa na Shirika la Kitaifa la Takwimu nchini Kenya (KNBS).

    Ripoti hiyo inaonyesha kuwa wakenya wengine 600,000 walilazimika kufanya kazi za kiwango cha chini zenye mshahara mdogo baada ya kutokuwa na kazi kwa muda mrefu.

    Kwa jumla,kati ya mwezi Oktoba na Disemba mwaka jana,kulikuwa na wakenya 929,595 ambao hawakuwa wameajiriwa,ikimaanisha kuwa hawakuwa na kazi lakini wamekuwa wakitafuta katika kipindi cha wiki nne kabla ya utafiti huo kufanywa.

    Kulingana na Ripoti hiyo,kiwango cha kitaifa cha ukosefu wa ajira kilikuwa asilimia 4.9 katika robo ya nne ya mwaka jana ikilinganishwa na asilimia 5.3 katika robo ya tatu ya mwaka huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako