Televisheni ya Afghanistan imetangaza kuwa mchakato wa kubadilishana wafungwa kati ya serikali na kundi la Taliban umeahirishwa kwa mara ya tatu. Habari zinasema mchakato wa kuwaachia huru wafungwa wa Taliban uliopangwa kufanyika alhamisi, umeahirishwa na huenda utatekelezwa jumamosi. Ujumbe wa Taliban uliwasili Kabul jumanne , na mazungumzo kuhusu kubadilishana wafungwa yalifanyika hadi alhamisi, lakini hakuna mambo halisi yaliyotangazwa kuhusu mazungumzo yaliyofanyika alhamisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |