Shirika la kuhudumia watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF limeshukuru msaada wa China kwa juhudi zake katika kuboresha huduma za afya kwa akina mama na watoto barani Afrika, hasa nchini Ethiopia.
Kwenye taarifa yake iliyotolewa jana Alhamisi, UNICEF imesema China kupitia shirika lake la misaada la kimataifa, Shirika la Ushirikiano wa Maendeleo la China CIDCA, imechangia dola za kimarekani milioni 1 ili kuboresha huduma za afya kwa watoto wachanga nchini Ethiopia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |