Rais Vladimir Putin wa Russia ametangaza kurefusha muda likizo yenye malipo kwa warusi wote hadi tarehe 30 mwezi Aprili kutokana na COVID-19.
Rais Putin alitangaza kwa njia ya televisheni kuwa, kama hali ikiruhusu, Russia itarekebisha kipindi kilichotangazwa cha siku za kutofanya kazi kutokana na mwelekeo wa kupungua kwa maambukizi.
Amesema majimbo yatafanya maamuzi kwa mujibu wa hali yake halisi, ni taasisi na mashirika gani yanayotakiwa kusimamisha shughuli zao au kuendelea na shughuli zao kwa msingi wa kuhakikisha usalama wa raia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |