• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • RIADHA: Aliyekuwa mshikilizi wa rekodi ya marathon akamatwa

    (GMT+08:00) 2020-04-03 17:16:53

    Aliyekuwa mshikilizi wa rekodi ya Marathon, Wilson Kipsang amekamatwa jana usiku na watu wengine 20 walipokuwa ndani ya klabu moja huko Iten kwa kukiuka amri ya kutotoka nje kuanzia saa moja usiku hadi saa kumi na moja alfajiri iliyowekwa na serikali ya Kenya, ikiwa ni jitihada za kupunguza kuenea kwa virusi vya Corona. Kamanda wa Polisi kaunti ya Elgeyo-Marawaket John Mwinzi amesema, Kipsang na watu hao walikamatwa saa mbili usiku baada ya maofisa wa polisi kuwakuta wakinywa pombe kwenye klabu hiyo maarufu baada ya saa moja usiku. Kipsang na wenzake hao walipelekwa kwenye kituo cha polisi cha Iten.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako