Mfumko wa bei nchini Uganda umepungua kwa asilimia 3 kufuatia kushuka kwa bei za nguo, viatu na nauli .
Hata hivyo haijulikani ikiwa bei hizoi zitaendelea kushuka au kuongezeka kwa sababu ya janga la Corona ambalo limeathiri maisha na uchumi kwa jumla.
Mkurugenzi mkuu wauchumi kwenye Taasisi ya Takwimu ya Uganda (Ubos) Bi Aliziki Kauda Lubega, alisema kupungua kwa mfumko wa bei unatokana na kushuka kwa jumla kwa bei kwa asilimia 2.5 kwa mwaka uliomalizika Machi ikilinganishwa na asilimia 3.1 kwa kipindi kama hicho mwezi uliopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |