• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Taasisi ya IFM Tanzania yapewa kazi ya kuandaa taarifa uwekezaji wa Pamba

    (GMT+08:00) 2020-04-09 19:22:43
    Wizara ya Kilimo nchini Tanzania imekipatia Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), kazi ya kuandaa taarifa ya kina ya uwekezaji katika viwanda vya zao la pamba ili kukuza soko lake.

    Aidha, imesema taarifa hiyo itatoa dira ya namna ya kuanzisha viwanda vikiwamo vya kusindika pamba na inatarajiwa kukamilika kabla ya Julai, 2020.

    Wizara hiyo ilitoa kauli hiyo bungeni jana wakati ikijibu swali la Mbunge wa Busega (CCM), Dk. Raphael Chegeni.

    Katika swali lake, Chegeni alisema zao la pamba linakabiliwa na kero nyingi kutokana na kukosekana uhakika wa bei yake.

    Kwa mujibu wa majibu ya Wizara hiyo, lengo la kazi hiyo ni kukuza soko la pamba na taarifa hiyo itatoa dira ya namna ya kuanzisha viwanda hivyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako