• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: Kampuni za nyumbani zaanza kutengeneza bidhaa za kujikinga kutokana na virusi vya corona.

    (GMT+08:00) 2020-04-20 16:28:43
    Halmashauri ya Vyakula na dawa ya Rwanda (FDA) yameidhinisha zaidi ya kampuni ya 20 za humo nchini, kuanza kutengeneza bidhaa za kujikinga dhidi ya virusi vya corona.

    Kampuni hizo zitatengeneza maski, magwanda ya madaktari na vizuizi vingine ili kusaidia serikali kuu kupunguza uagizaji wa bidhaa hizi kutoka mataifa ya nje.

    Kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa Halmashauri ya vyakula na dawa, Dkt Charles Karangwa, kampuni hizo tayari zimepewa ruhusa ya kuanza shughuli hiyo baada ya ukaguzi wa kina. Baadhi ya kampuni zilikuwa tayari zikitengeneza bidhaa hizi, ila bila idhini. Lakini kwa sasa, wamepewa fursa hiyo kuendelea na kazi hiyo. Kwa jumla, kampuni hizi zinatarijwa kutengeneza takriban maski 600,000 kila siku.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako