Makadirio ya hivi karibuni ya Mfuko wa Fedha Duniani imeweka Kenya na Tanzania mwaka huu, viwango vya ukuaji wa uchumi wa Pato la Taifa kwa asilimia moja na asilimia mbili kwa mtiririko huo, chini kutoka asilimia 5.6 na 6.3 kwa mtiririko huo mwaka wa 2019. Uganda itadumisha viwango vya ukuaji wa Uchumi vya asilimia 3.5 ikilinganishwa na asilimia 4.9 mwaka 2019.
Lakini maoni ya mwaka 2021 ni bora kidogo kwa Uganda, Kenya na Tanzania, huku kiwango cha ukuaji Nairobi kinatarajia kupunda hadi asilimia 6.1 (juu kuliko 2019) wakati Tanzania na Uganda zikiponea na kufikia asilimia 4.6 na 4.3 kwa mtiririko huo.
IMF imesema janga la Covid-19 litasababisha usumbufu wa asilimia tatu katika uchumi wa dunia mnamo 2020, ambayo ni mbaya zaidi kuliko wakati wa mgogoro wa kifedha wa 2008-2009.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |